Iringa, Miaka ya hivi karibuni zao la muhogo limekuwa likitumika kwa usafi zaidi na hata kuwa zao la biashara jambo ambalo litawafanya wakulima wa Tanzania kuwafikia wakulima wa Afrika Magharibi ambapo wameanza kusindika zao hilo kwa muda mrefu na kufanikiwa kiuchumi.
Hapo awali zao la Muhogo kwa wananchi walio wengi lilkuwa linachukuliwa kama la kinga dhidi ya njaaa.
Utafiti uliofanyika nchini Italia kuhusiana na zao hilo unaonyesha kuwa muhogo unaweza kutumika kwa matumizi zaidi ya 300 yakiwemo unga wa muhogo, tambi, biskuti, mafuta ya lishe, keki, sabuni ya unga, kuni, mboga, pamoja na bidhaa nyingine nyingi.
Maofisa ugani wakieneza elimu ya kisasa ya kusindika muhogo katika maeneo mengi nchini zao la muhogo litakuwa ni zao kubwa na lenye heshima katika kuinua uchumi na kipato cha mkulima kwa kulifanya kuwa zao la chakula na biashara.
Takwimu kutoka Shirika LA Taifa la Utafiti wa Kilimo isiyo ya IITA inaonyesha kuwa uzalishaji wa zao la muhogo umefikia wastani wa tani 30,000 tu kwa mwaka uzalishaji ambao bado upo chini kutokana na wakulima wengi kukosa utaalamu wa kulisindika zao hilo.
Taarifa ya Shirika la Utafiti wa kilimo IITA inaonyesha kuwa zao la muhogo linastawi kirahisi.
Hii ni pamoja na kuvumilia ukame na halishambuliwi na magonjwa au wadudu wanaoathiri mazao mengine na pia muhogo unaweza kutoa mazao mengi katika ardhi duni ambayo mazao kama mahindi hayawezi kustawi.
Kwa mujibu wa IITA, muhogo ni zao la pili kuwa na wanga mwingi baada ya viazi vitamu ambavyo vina asilimia 20 hadi 30 ya wanga na kwamba asilimia 84 ya zao hilo hutumika kama chakula cha binadamu.
Aidha, katika baadhi ya maeneo zao hilo hutumika kama chakula cha mifugo na sehemu kidogo ya zao hilo husafirishwa nje ya nchi.
Zao la muhogo lina mizizi inayotoa wanga, unga na nishati wakati majani ya mhogo ni chakula kizuri chenye vitamini, protini na madini ya chuma ambayo ni muhimu kwa afya ya binadamu.
Utafiti unaonyesha kuwa Tanzania ni moja ya nchi ya wazalishaji wakubwa wa muhogo duniani ambapo katika bara la Afrika, Tanzania inachukua nafasi ya nne baada ya Nigeria, Ghana na Kongo DRC.
Kutokana na hali hiyo Tanzania ina fursa kubwa ya kuongeza uzalishaji wa zao la muhogo hata kuwa nchi ya kwanza katika bara la Afrika kutokana na kuwa na utajiri wa ardhi kubwa yenye rutuba.
Takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania inazalisha muhogo kwa wastani wa tani mbili tu kwa mwaka kwa hekta na wastani wa bara la Afrika ni tani 3.3 kwa mwaka, wastani wa Nigeria ni tani 4.7 kwa mwaka.
IMEANDALIWA NA ZAINA MALOGO
0 comments:
Post a Comment